MFULULIZO WA MASOMO YA MISINGI YA IMANI YA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO.
10: MSINGI WA KUMI - UZOEFU
WA WOKOVU.
Uzoefu wa wokovu ni
safari ya maisha ya mwenye dhambi akipitia hatua au njia mbalimbali mpaka
afikie wokovu. Njia hizo ni; kuamini, kutubu, kuungama, kusamehewa, kuhesabiwa
haki na kutakaswa.
FUNGU
KUU: “ kwa maana mmeokolewa kwa neema,
kwa njia ya imani;ambayo hiyo haikutokana na
nafsi zenu, ni kipawa cha MUNGU” Waefeso 2:8.
- Neema ni nini? Waefeso 2:8
Maelezo: Neema-Ni “huruma na upendo tele wa Mungu unaookoa wenye dhambi
wasiostahili kuupata kama ulivyofunuliwa
katika kristo. Ni upendo unaobadilisha, usio na mipaka na unaohusisha wenye
dhambi wajinsi zote. Neema hii siyo tu huruma ya Mungu inayomfanya akubali
kumsamehe mwenye dhambi, bali in nguvu ya kuokoa”. Kwa maneno mengine NEEMA ni
huruma, wema na fadhili ya Mungu kwa binadamu asiye stahili kuokolewa.
- Imani ni nini? Waebrania 11:1
Maelezo: Imani ni sifa na
hali ya kumtumaini Mungu kwa kuamini kwamba anatupenda na anajua zaidi kile kilicho
na faida kwetu. “Imani ni kuwa na hakika ya mambo yasiyoonekana na ni bayana ya
mambo yatarajiwayo”.
- Imani inayoleta wokovu ni ipi? Yahana 3:16
Maelezo: kwavile zipo imani za aina nyingi sana, wanatheologia wanaitafasiri
imani inayoleta wokovu kama “imani iletayo wokovu siyo ile yakuwezesha kukubali
ukweli tu, ni imani inayompokea kristo kama
mokozi binafsi ikiwa na uhakika kwamba YESU anaweza kuwaokoa wote wanaokuja kwa
Mungu kupitia kwake. Mtu anapomtegemea YESU kama tumaini lake pekee
la wokovu basi hapo imani ya kweli imejifunua”.
- Ni kwanjia gani tunapata imani? Warumi 10:17,9-10.
“Imani huja kwa njia ya kusikia, na kusikia huja kwa njia ya neno la
Mungu.” “Ikiwa utakiri kwa kinywa chako, kuwa YESU ni Bwana na kuamini kwamba
Mungu alimfufua toka katika wafu utaokolewa. Kwakuwa ni kwa moyo wako unaamini
na kuthibitika, na nikwakinywa chako
unakili basi utaokolewa.”
- Imani na injili: Ili mtu aokolewe sharti afanye nini? Warumi 1:16.
“kwakuwa siionei haya injili, kwasababu ni uweza wa Mungu uletao
wokovu, kwa myahudi kwanza na kwa myunani pia.”
B: KUTUBU.
FUNGU
KUU: 1Yhana 1:9
“Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wahaki hata
atusamehe makosa yetu na kutusafisha na udhalimu wetu wote.”
1.
Je, kutubu ni
lazima katika mpango wa wokovu? Matendo 17:30
Maelezo: “kutubu ndiyo hatua ya kwanza ambayo ni lazima kuchukuliwa na wote
ambao wanataka kumrudia Mungu. Inatupasa kila mtu anyenyekeze moyo wake mbele
za Mungu na kuacha nia yake mbaya.
2.
Mtu anaweza
kufanya nini ili dhambi zake zisafishwe? Matendo 3:19
Maelezo: Maranyingi tunahuzunika kwasababu matendo yetu maovu yanatuletea
matokeo mabaya kwetu sisi wenyewe, lakini hii sio toba. Huzuni halisi ya dhambi
ni matokeo ya kazi ya Roho Mtakatifu. Kila dhambi humtonesha YESU vidonda
vyake, na tunapo mtazama YESU, ambaye sisi tuliomuumiza tunaomboleza kwa sababu
ya dhambi zilizomletea maumivu. Maombolezo hayo yanatuongoza kuacha dhambi.
3.
Wenye dhambi
wanaongozwaje kwenye kutubu? Warumi 2:14" Kwa
maana watu wa mataifa wasio na sheria wafanyapo kwa tabia zao yaliyo
ndani ya torati, hao wasio na sheria wamekuwa sheria kwa nafsi zao
wenyewe." hivyo kuna nguvu isiyo ya kawaida inayokusukuma kutenda kwa
namna ya sheria japo huijui sheria yenyewe. mfano mtu asiye na sheria ya
Mungu hawezi pia kumuoa au kuolewa na Mama au Baba yake, kwa tabia hiyo
imekuwa sheria kwake. je, ametambuaje kufanya hivyo kuwa si vyema?
4.
Jambo
gani linalofuata ungamo la kweli? Mithali 28:13
Maelezo: Ungamo haliwezi kukubaliwa na Mungu pasipo toba na matengenezo ya
dhati. Nilazima pawepo mabadiliko ya lazima katika maisha, na kila kinacho
muudhi Mungu lazima kiachwe kabisa. Jambo hili litakuwa na matokeo ya huzuni
halisi ya dhambi.
5.
Kuungama
kungalifanywa kwa nani? Zaburi 32:5
Maelezo: Ungameni dhambi zenu kwa Mungu ambaye yeye tu ndiye awezaye
kuzisamehe. Namakosa mliyokoseana nyinyi kwa nyinyi ungamanianeni nyinyi kwa
nyinyi ili Baba yenu wa mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Ukimkosea ndugu
yako au jirani yako itakubidi kulikubali kosa lako na niwajibu wake kukusamehe
bure. Ndipo unapaswa kuomba msamaha kwa Mungu wa Mbinguni, kwasababu huyo
nduguyo uliyemkosea na kumuumiza ni mali ya Mungu. Na kwa kumuumiza
ulimtenda dhambi Muumbaji na Mokozi wake.
6.
Kuna ahadi
gani juu ya dhambi ambazo zimeungamwa? Ebrania 8:12, ".....nitawasamehe maovu yao, na dhambi zao sitazikumbuka tena."
7.
Mtu ambaye
amesamehewa dhambi zake anakuwa na hali gain? Zaburi
32:1,2
"Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake. Heri BWANA asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila." ukisamehewa dhambi zako utakuwa na amani moyoni kwani hutakuwa na hatia inayokusuta rohoni mwako.
"Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake. Heri BWANA asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila." ukisamehewa dhambi zako utakuwa na amani moyoni kwani hutakuwa na hatia inayokusuta rohoni mwako.
8.
Kusamehewa
kwetu na Mungu kunategemea vipi uhusiano kati yetu na wengine? Marko 11:25 - 26
" Nanyi, kilamsimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu." Mathayo 6:14,15. Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu."
" Nanyi, kilamsimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu." Mathayo 6:14,15. Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu."
9.
Je, Mungu
atakumbuka dhambi zetu baada ya kutusamehe? Yeremia
31:34.
"........asema BWANA; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena." Ebrania 8:12, Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena."
"........asema BWANA; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena." Ebrania 8:12, Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena."
10.
Je,Mungu
atasamehe dhambi kiasi gain? Isaya 1:18
" Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu."
" Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu."
MWISHO:
This scriptures should be considered to be more spiritual than social.
ReplyDelete