Thursday, 20 December 2012

MAHUSIANO SAHIHI...2


TANZANIA HIGHER LEARNING INSTITUTION SEVENTH-DAY ADVENTIST STUDENT ORGANISATION (THISDASO), DODOMA ZONE.

IDARA YA MAMBO YA KIROHO – KANDA YA DODOMA.

Tarehe 02 – 10/06/2012.


Karibuni wageni Kwa wenyeji tuyachunguze maandiko.


SOMO LA KWANZA: MAHUSIANO SAHIHI.

SEHEMU YA KWANZA. Juma Pili - 03/06/2012.
 
UTANGULIZI
Maana ya uhusiano, Uhusiano ni neno pana sana kutegemea mahali linapotumika, kamusi ya Kiswahili sanifu inaeleza uhusiano kuwa ni hali ya kuwa na mfungamano.Kuna uhusiano mzuri au sahihi na uhusiano mbaya. Uhusiano ni tabia ya MUNGU, YESU anasema Mimi na BABA tu umoja” Yoh 10:30,kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni; Baba, Neno na Roho Mtakatifu na hawa wote ni umoja” 1Yoh 5:8, umoja kati ya nafsi hai za uungu ni udhihirisho wa uhusiano mtakatifu katika tabia na utendaji kati ya MUNGU Baba, Mwana na Roho mtakatifu.

Kwa kuwa mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa MUNGU aliumbiwa tabia hii ya kuhusiana, wataalamu wa sayansi ya jamii wanasema mwanadamu ni kiumbe aliyeumbwa kuishi kijamii yaani  kwa mahusiano na wengine, furaha ya mwanadamu inakamilishwa kwa uhusiano kati yake na MUNGU muumbaji,uhusiano kati yake na wanadamu wengine na uhusiano wake na vitu vilivyo mali ya MUNGU, hakuna furaha ndani ya mwanadamu asipofungamana ama kuhusiana na MUNGU muumbaji, wanadamu wenzake na vitu  vingine alivyoviumba MUNGU.

Kabla ya dhambi kulikuwa na uhusiano mzuri na sahihi kati ya Adamu na Hawa na muumbaji wao, waliongea naye uso kwa uso kama rafiki yao waliishi na viumbe vyote katika bustani kwa furaha wakicheza na simba, dubu, nyoka lakini pia wao kwa wao walijawa na furaha na amani tele kila wakati.
Baada ya dhambi hali ya mambo ilibadilika MUNGU hakuongea nao tena uso kwa uso, wanyama na viumbe vingine vikawa adui zao na maisha yao yakajawa na huzuni na simanzi tele.

Hata hivyo, kwa kuwa MUNGU ni mwenye upendo alianzisha na kumfundisha Mwanadamu kanuni za msingi za mahusiano ambazo zikipokelewa na kufanyiwa kazi zitaleta furaha na ustawi bora kwake.

A: KANUNI KUU ZA UHUSIANO SAHIHI
1.   Utii kwa sheria na maagizo ya Mungu;  uhusiano unaendeshwa katika misingi ya utii kwa neno la mungu na sheria yake, ndio uletao furaha, bali uhusiano uliojegwa katika kuridhishana na kufurahishana kwa kitambo, huku amri takatifu na maelekezo ya neno la mungu yakivunjwa, huishia kwenye huzuni na hata kuvunjika, “mkikubali  na kutii mtakula mema ya nchi bali mkikataa na kuasi mtaangamia kwa upanga’’ Isaya 1:20,mitume na ndugu wakasema imetupasa  kumtii MUNGU kuliko wanadamu” (matendo 5:29) kwa ujumla uhusiano wowote unaomuondoa MUNGU ili kuimarisha uhusiano kati ya mwanadamu na mwanadamu au mwanadamu na mali hauzai matunda ni sawa na mti uliokatwa na kuchimbiwa katika udongo usio na maji, utaonekana na majani mabichi kwa kitambo tu kisha utanyauka.

2.   Upendo wa kweli; Bwana yesu alithibitisha kanuni hii ya uhusiano aliposema, mpende MUNGU wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote, hii ndiyo amri ya kwanza iliyo kuu, na ya pili yafanana nayo, mpende jirani yako kama nafsi yako: (mathayo 22:27-30) angalia pia (Luka 10:27), upendo wa kweli ndiyo gundi ya uhusiano wa aina yoyote, uwe ni urafiki, uchumba, ndoa, kazini, nyumbani na sehemu yoyote. Upendo huambatana na matendo yote mema yanayoimarisha uhusiano kama adabu, uvumilivu, utu wema, fadhili, kuaminiana, kuthaminiana n.k na kuondoa matendo yote mabaya yana haribu uhusiano kama majivuno, husuda, kuhesabu mabaya, kutokuheshimiana, kutokuthaminiana n.k (1 kor 13:1-10).

B: AINA ZA MAHUSIANO:
Kuna aina nyingi za uhusiano au mfungamano katika jamii, baadhi ya mifano yake ni; urafiki, undugu, uchumba, ndoa na kadhalika. Mifungamano au mahusiano haya yaweza kuwa kazini, nyumbani, chuoni, kanisani na mahali pengine panapokutanisha watu pamoja (social agent). Aina zote hizi za mahusiano zitadumu na kumletea mwanadamu furaha ya kweli ikiwa zitazingatia kanuni kuu mbili za uhusiano wa ukweli yaani utii kwa sheria na maagizo ya MUNGUna upendo wa kweli. Katika aina zote za uhusiano, uchumba na ndoa ndizo zenye changamoto nyingi na na wengi wamekosea katika Nyanja hii, hivyo badala ya kupata furaha kama walivyokusudia wameishia kwenye majuto, simanzi na huzuni maisha yote. Hebu tuangalie baadhi ya ushauri wa neno la MUNGU katika aina hizi za uhusiano.

I: UCHUMBA:
Uchumba ni uhusiano halali na unaoungwa mkono na biblia ikiwa utafanyika kama neno la MUNGU linavyoelekeza. Biblia inasema Mwezi wa sita malaika Gabrieli alitumwa na MUNGU kwenda mpaka mji wa Galilaya jina lake Nazareti kwa mwanamwali Bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu, wa mbali ya Daudi na jina lake Bikira huyo ni Mariamu”.
Hivyo utaratibu wa kuposana au kuchumbiana umekuwepo hata nyakati za biblia miongoni mwa wakristo waaminifu kama Yusufu na Marium soma pia mathayo 1:18.
Kanuni ya kanisa inasema uchumba ni kipindi cha maandalizi kwa vijan waliopendana kuoana. (soma kanuni ya kanisa sura ya 13 uchumba na ndoa).
Kwa hiyo kama kanuni za neno la MUNGU zikifuatwa uchumba ni uhusiano mzuri uliokusaidiwa kuwaletea furaha wahusika katika kipindi chote cha uchumba na katika maisha yao ya ndoa, kinyume chake kanuni za neno la MUNGU zinapokiukwa wahusika hujiletea huzuni na majonzi wakati huo wa uchumba na katika maisha yote ya ndoa ikiwa wanafanikiwa kuonana, na kuukosa uzime wa milele kama wahusika wasipogeuka na kurudi kwa mwokozi yesu kristo kwa msaada.

Ili kijana aweze kupata furaha na heshima maishani yapo mambo 10 ya kuzingatia katika uhusiano wa uchumba.

MAMBO 10 YA KUZINGATIA KATIKA UHUSIANO WA UCHUMBA.
I:USIHARAKISHE.
Usiharakishe na kukurupuka kutafuta mchumba kabla ya wakati muafaka.Pengine unaweza kujiuliza ni wakati upi ni muafaka kutafuta au kuwa na mchumba?ni wakati unapokuwa umekomaa kiroho, kiakili na kimwili umejitambua kikamilifu ulikotoka, mahali ulipo na unapokwenda na umetathimini kwa makini mipango na ratiba yako ya sasa na ya baadaye ndipo waweza kuchukua hatua hii mhimu katika maisha.
Wengi wamepuuzia hili na kukurupuka kutafuta mchumba bila kujitathmini na kuishia kwenye uasherati na usaliti vilivyowaletea huzuni na majuto badala ya furaha na ndoa takatifu. Biblia inasema Ni nani katika ninyi Kama akitaka kujenga mnara asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama kwamba anavyo vya kumalizia asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi watu wote waonao wakaanza kumdhihaki…….” (Luka 14:28-30).

II: USITAFUTE MCHUMBA KWA MSUKUMO KUTOKA NJE.
Usitafute mchumba Kwa kuangalizia, kushawishiwa, kuiga au kusukumwa na ndugu, marafiki au washiriki wenzako, suala la kutafuta mchumba linapaswa kutoka ndani yako baada ya kujithamini na kuona kuwa ni wakati mwafaka na kupata sababu za msingi za kupata mchumba hatimaye kufunga ndoa.

III: USITAFUTIWE MCHUMBA.
Vijana wa kiume na wa kike wanatakiwa kuwa makini sana katika suala hili, yakupasa uwe na orodha yako ya sifa unazozitaka, cha msingi zisipingane na neno la MUNGU, hizo zitakuongoza katika kutafuta mke au mme utayempenda na kumfurahia, fanya maamuzi ambayo hutakuwa na sababu ya kumfurahia mwingine.
Ushauri wa ndugu, jamaa, marafiki na viongozi wa kanisa unafaa kuzingatiwa kwa makini,lakini maamuzi ya mwisho yatoke kwa mhusika ambaye ataambatana na huyo mwenzi maisha yote, wengi wametafutiwa na kuishia kulaumu na kuvunja uchumba na hata ndoa.

IV: USIFANYE UCHUMBA WA SIRI.
Uhusiano kati ya kijana wa kiume na wa kike waliopendana, waliokubalian kuoana huitwa uchumba baada ya vijana hao waliokubaliana kuwajulisha wazazi wa pande zote mbili na ikibidi viongozi wa kanisa. Kuendesha mahusiano ya siri siri kunafananishwa na Nabii sawa na dhambi ya wizi, kuiba upendo wa msichana, kwa kweli kitendo hiki hakikubaliki kabisa na si chema kwa binti mwenyewe, kwa wazazi na hata mbele za MUNGU(soma kuchagua mchumba uk 23, soma pia Nusuru ndoa yako uk 107 “mvulana ampendaye msichana …. Bila kujulikan kwa wazazi wa msichana hafanyi tendo jema kwa msichana mwenyewe wala kwa wazazi wake. Kwa kweli hata hafanyi kitendo chema cha kikristo (kuchagua mchumba uk 23) madhara ya uchumba wa siri ni pamoja na kuvunja uhusiano wenu na MUNGU, kukosa ushauri wa wazazi na viongozi wacha MUNGU, kufasiriwa vibaya na watu wanaowaona na kujiingiza katika vitendo viovu vya uasherati kwa urahisi. Hivyo mara baada ya kukubaliana, ni muhimu kutoa taarifa kwa wazazi na uongozi wa kanisa.

V:USIWE NA WACHUMBA WENGI.
Ajifanyiae rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe……..” (Mithali 18:24). Utafiti unaonyesha kuwa vijana wengi wa kiume na wa kike wakristo huwa na wachumba wengi kwasababu kwa sababu zifuatazo, kwanza kutokuwa na uhakika kuwa yupi mchumba wa kweli, pili ni kutaka kupata umaarufu, tatu ni tamaa na nne ni kutaka vya bure na tano ni kukurupuka. Hiyo siyo tabia njema kwa kijana mkristo, kuwa na wachumba wengi kuna madhara makubwa. mfano kuwa mdanganyifu ili kuwaridhisha wote, kusababisha ugomvi na hata kuuana miongoni mwa wa wapenzi wako, wakigundua wote waweza kukuacha, lakini pia ni kuwapotezea muda wengine.Mungu hapendezwi na mwenendo huo hata kidogo,uovu  huu usipoachwa, utajitokeza tena katika maisha ya ndoa baada ya harusi (kuchagua mwenzi uk 23) muombe MUNGU kwa imani uwe naye mmoja tu kwa wakati na inaposhindikana, tulia mwombe MUNGU naye atatuongoza mahali sahihi.

VI: USIOMBE UCHUMBA KWA MAJARIBIO “KUUDHIHAKI MOYO”
Kudhihaki ni kosa ambalo halina upungufu wowote machoni pa MUNGU mtakatifu. Ingawa ni hivyo wengi huonyesha wasichana mapenzi na kuamsha upendo wao na baadaye wakaenda zao bila kujali Waliyonena na bila kufikiri maneno yao yatakuwa na matokea gani kwa yule msichana. Wanapokuwa wakitangatanga huko na huko huona sura mpya…. Na kuamsha mapenzi ya msichana mwingine hali kadhalika wakaenda na kumsahau pia. Vile vile wako wasichana wenye mienendo kama hiyo (kuchagua mwenzi uk 23) huu ni ouvu mbele za MUNGU, wengi wamejinyonga na kunywa sumu kwa sababu ya dhihaka za vijana ambao hawakua na dhamira ya dhati, waliotamka nakupenda  kwa majaribio  au kwa lugha inayotumiwa na vijana kujipima uzito, kisha wakaenda zao. Hebu kijana usiombe uchumba ikiwa huja dhamiria, wala usiombe uchumba bila kupenda au kwa kumsaidia msichana ama kumkubali kijana kwa kumsaidia au kwa majaribio, hiki si kitendo chema kabisa kwa anayetendewa na mbele za MUNGU.

VII: USIWE MWONGO, MUELEZE UKWELI WOTE KUHUSU WEWE.
 “Nao ulimi ni moto, ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi umewekwa katika viungo vyetu na ndio uutiao mwili wote unajisi; huuwasha moto mfululizo wa umbile nao huwashwa moto wa jehanamu” (Yakobo 3:6) kama kuna kitu kinachoweza kuteketeza uchumba wako ni uongo na usengenyaji. Vijana wengi hutafuta mchumba kwa uongo kwa kujipatia sifa au hadhi zisizo za kweli na kuficha baadhi ya mambo mhimu yanayowahusu, uwe wazi kwa mchumba wako au kijana anayetarajia awe mchumba wako.Ikiwa una mtoto au ulishawahi kuoa au kuolewa.Mueleze mipango au njozi zako za baadaye ili anapofanya maamuzi ya kuwa na wewe awe ameridhika na awe tayari kuwa na wewe jinsi ulivyo, huu ndio msingi wa upendo wa kweli.

VIII: EPUKA VITENDO VINAVYOWEZA KUTAFSIRIWA VIBAYA
 Biblia inasema sisi ni barua iliyoandikwa na kusomwa na watu wote”(2kor 3:2-3), kwa kuwa sisi ni barua ya  MUNGU kwa watu wanao tuzunguka imetupasa kuepuka vitendo vyote vinavyoweza kutufanya tusomeke vibaya.Miongoni mwa vitendo hivyo ni kukaa mazingira ya kificho mfano gizani,chumbani au vichakani, watu wakiwaona wanawatafsiri vibaya na hivyo kuwazuia kumuona kristo katika maisha yenu,pamoja na hayo  mazoea haya ndio chanzo kikubwa kuelekea katika uzinzi na uasherati .Kitendo kingine ni kuwa pamoja kila wakati ,ninyi sio mume na mke,huu sio wakati wake, kitendo hiki husababisha vijana kuzama katika mapenzi mazito kabla ya wakati,na hivyo huwa vipofu wa mapenzi,hiki nacho ni kichocheo kikubwa cha ngono kabla ya ndoa,kitendo kingine ni maongezi usiku wa manane, tabia hii haimpendezi mungu,saa za usiku ni saa za kumpumzika,kukesha usiku kucha kwa ajili ya maongezi kunadhuru afya yenu vilevile,madhara yake ni pamoja na kudhoofu ubongo,uchovu mwingi na hivyo kufanya hata ufanisi wa kazi zako upungue,pia kitendo hiki huamsha tama za mwili na mwisho kutumbukia katika zinaa na uasherati,na ukiwa unazungumza chumbani unakera wengine na wanakutafsiri vibaya.Tabia nyingine ni  kutumia pesa au zawadi nyingi ili kuimarisha uchumba au kupata mchumba,kitendo hiki pia si mpango wa MUNGU,uchumba unapaswa kujengwa katika msingi wa upendo wa kweli na si vitu.Tabia hii husababisha upofu wa mapenzi hivyo mambo muhimu hupuuzwa na wengi hujitumbukiza katika uhusiano wa ndoa na watu wasiofaa.

IX: EPUKA ZINAA NA UASHERATI.
Azinie na mwanamke hana akili kabisha (Mithali 6:32), Vijana wengi hudhani ngono kabla ya ndoa  ni ujanja na huimarisha uhusiano wao.Lakini hiki ni kitendo kinacho haribu kabisha uhusiano wako na mwenzi wako na uhusiano wenu na mungu.Aidha uzinzi na uasherati unamadhara na hasara zake hasa kwa wasichana.Baadhi ya hasara wazipatazo wasichana ni kama zifuatazo:
Kupata mimba nje ya ndoa (mimba sizizotarajiawa), kukakataliwa na wachumba wao,kuharibu uwezakano wa kupata mchumbamwingine tena,vifo kwa sababu ya kujaribu kutoa mimba walizo pata bila ya kutegemea,kupoteza heshima katika jamii,kuvunja uhusiano wao na MUNGU n.k Sasa kwa nini usiepuke mambo haya kwa kuwa mwaminifu?

X: USICHUMBIE MTU WA IMANI TOFAUTI NA WEWE.
 Msifungiwe nira na wasioamini kwa jinsi isivyo kawaida” (2 kor 6:14), kuonana na kijana mwenye imani tofauti na wewe kunaleta migogoro mizito na isiyokoma katika maisha ya ndoa.Mungu amezuia jambo hili tangu zamani ,akawaelekeza waisraeli taifa lake teule wakati ule alisema wale msioane nao, binti yako usimpe mwanawe mume, wala msimtwalie mwanao mume binti yake (kumb 7:2,3).Sababu yake Mungu anasema kwa kuwa atamkengeusha mwanao asimfuate Mungu ili wapata kuabudu miungu mingine(kumb 7:4) Vijana wengi wameyapuuza maagizo haya mema na kuongozwa na tama za mioyo yao kama ilivyokuwa kwa Samsoni(waamuzi 14: ) wengine wakidai watawaongoa , huku ni kujidanganya ,Suleimani alikuwa na hekima kuliko watu wote wa wakati wake na wakati huu, alifanya kosa hilo hilo akitaka kuongoa mataifa yaliyomzunguka kwa kuoa binti zao lakini mwisho aliishia anguko kuu la kiroho na kugeukia miungu yao Suleimani akawapenda wanawake wengi wageni nao wakaugeuza moyo” (1fal 11:) kama Suleimani alishindwa, vipi wewe?, anaweza kukubali ili kukuridhisha na kukupata wewe lakini kwa hakika huo sio uongofu wa moyoni na matokeo yake utayashuhudia baadaye.Ndoa zimegeuka kuwa mahabusu na jela ndogo,migawanyiko ya imani,malumbano yasio koma,ugomvi usio koma, kwa sababu watu wawili wenye itikadi na falsafa mbili tofauti waliunganishwa  kwa ndoa bila ya kujali mausia ya neno la Mungu.Kijana ikiwa uliingia katika mausiano ya namna hii bila kujua au kwa kujua kwa neema ya yesu na hekima ya mbinguni vunja uhusiano huo mara moja.

SEHEMU YA PILI: Juma Tatu – 04/06/2012.
II: NDOA.
 Ndoa na iheshimiwe watu  wote na malazi yawe safi (Ebrania 13:4) kama tulivyo tangulia kusema kanuni kuu mbili zinazoweza kuleta furaha katika mahusiano yoyote ni kutii sheria na maagizo ya neno la Mungu na upendo wa kweli,Furaha ya ndoa hupatikana pale tu wanandoa watakapoamtanguliza na kumheshimu Mungu katika maisha yao ya ndoa, kadri tunavyomkaribia Mungu ndivyo tunavyo karibiana sisi kwa sisi, biblia inasema Bwana asipoijenga nyumba  waijengao wafanya kazi bure, na Bwana asipoulinda mji waulindao wakesha bure (zab 127:1) ,hivyo kumtii Mungu na upendo wa ukweli kati ya wana ndoa  na kati yao na Mungu ndizo kanuni kuu katika maisha ya ndoa kwa maelezo yenye ufafanuzi, napenda kumnukuu mshauri mkongwe wa ndoa na mwandishi wa kitabu cha nusuru ndoa yako.Pastor Daudi Makoye, juu ya sheria kumi za kulinda uhusiano na mwenzi wako na kanuni kumi za ndoa.

      A: SHERIA KUMI ZA KULINDA UHUSIANO NA MWENZI WAKO
i)             Chunga ulimi wako, daima sema machache kuliko unavyofikiri.
ii)           Timiza ahadi hatakama inagharimu.
iii)         Usikose nafasi ya kusema neno linalolitia moyo kwa siku.
iv)         Uvutiwe na mume au mke wako kwa yale afanyayo.
v)           Usibishane naye.
vi)         Zuia kusema ovyo kasoro za mwenzako.
vii)       Uwe mwangalifu usimkwaze mwenzako katika hisia.
viii)     Usijali maneno yanayopelekea kukuumiza.
ix)         Usimdanganye mwenzi wako.
x)           Fanya kazi, vumilia na fanya mambo yote yawe ya kupendeza.

B: KANUNI KUMI ZA NDOA.
i)             Usiwe na mke au mume mwingine ila Yule uliye funga naye ndoa.
ii)           Usijifanyie wapenzi wengine mfano wa mume au mke wako, usiwahusudu wala kuwatumikia.
iii)         Usimtaje ovyo ovyo mume wako au mke wako kwa majirani au ndugu usije ukadharaulika wewe na mkeo.
iv)         Ikumbuke siku ya harusi uiheshimu na kuisheherekea wewe mkeo na wanao.
v)           Waheshimu wakwe zako ipasavyo.
vi)         Usiue pendo lenu.
vii)       Usizini.
viii)     Usiibe haki ya ndoa na mali yenu.
ix)         Usimshudie uongo mume wako au mke wako.
x)           Usitamani mke au mume wa mwenzako

Haya ni baadhi ya mambo au ushauri unaoweza kusaidia kuimarisha uchumba na ndoa zetu. Lakini jambo kubwa ni kumfanya KRISTO awe mkuu na mwenyeji wa uchumba wetu na ndoa zetu wala tumsimfanye mgeni asiye na uhuru au mamlaka katika uchumba wetu au ndoa zetu.

Napendekeza kwenu kitabu cha Pastor Makoye “Nusuru ndoa yako’ na Pr.Mange “It is not goodKuchagua mchumba cha E.G.white Kisomwe na kila kijana na mwanandoa,ni hazina iliyositirika.

MJADALA WA MASWALI YA PAMOJA.
Mwendesha somo awashirikishe wanadarasa kwa nafasi ya kujadili mambo yaliyozungumzwa hapo juu kwa pamoja ili kupanua uelewa na kutiana moyo kufanya mahusiano yaliyosahihi mbele za MUNGU.

SOMO LA TATU:          MAVAZI NA MVUTO.  
[ 1Timotheo 2;9,10, 1Petro 3;3-5 ].
SEHEMU YA KWANZA.     
UTANGULIZI:
Tumezungukwa na ishara kila mahali, lugha zetu, utamaduni, jamii, siasa kila kitu kwa kiwango Fulani hutujia vikiwa katika mfumo wa ishara; bendera, nembo, picha na kauli mbiu, sanaa , mashairi, na taratibu za ibada hutumika kutegemeana na mahali; hivyo vyote huwa na maana kubwa kuliko vitu vyenyewe.

USAFI WA MWILI.
Katika kutunza mwili wako ili uvutie, hautaishia kwenye vyakula tu na kuupatia mahali pa kulala; unahitaji pia utunzaji wanje. Suala hili la utunzaji wa mwili na usafi wa nje ni la muhimu sana hasa kwa wasichana. Wavulana nao wanaguswa sana na usafi wa nje, ingawa ukilinganisha kati ya wasichana na wavulana utagundua kwamba wasichana  wanaguswa zaidi kuliko wavulana, na ndiyo maana hakuna mvulana atakayevutiwa na msichana  mwenye kamasi, anayenuka mdomo, kwapa, chawa kichwani, mafuta yenye harufu mbaya kichwani na katika marinda ya magauni yaliyopitwa na wakati.

Hali hii ya uchafu wa nje, hufanya sifa ya tabia njema ya ndani isionekane kwa msichana au mvulana, mwonekano wa nje ndio unaochagia msichana kuposwa na ndiyo maana siku hizi wasichana wanakazania urembo na kusahau urembo wa tabia zao, usafi wa nje na ndani visitenganishwe na vile vinavyoonekana kwa nje, iwe hivyo na ndani pia au vile ulivyo kwa ndani, ionekane hivyo na nje pia.

Ukilejea katika kitabu cha Ruth 3:3, Naomi alimwambia Ruthu Basi wewe oga, ujipake mafuta, ujivike mavazi yako kisha uende kwenye uga”. Katika usafi hapa, Ruthu aliambiwa kufanya mambo matatu ambayo hata vijana wa leo wanaambiwa kuyafanya nayo ni (a) Aoge (b) Apake mafuta (c) Avae mavazi.

Miili yetu imeumbwa kwa kuwa na viungo vingi, lakini kuna viungo ambavyo macho ya watu yanaweza kuviona kirahisi. Vipo viungo ambavyo vinaweza kuonekana kirahisi. Vipo pia viungo ambavyo vinaweza kujificha  lakini viungo kama; meno, mdomo, pua, masikio, macho, nywele , miguu na vidole vya mikono havifichiki. Viungo hivi vinaweza kukudhalilisha na kuharibu haiba usipoviweka katika usafi wa kutosha, Na sasa tuanze kuangalia kiungo kimoja baada ya kingine.
Kama waadventista tunaelewa lugha ya biblia inavyotumika kuwakilisha kitu fulani
v  Somo hili linalenga katika mifano ya Biblia ya namna mvuto na mwonekano wa mkristo wa kweli waweza tambulishwa na kielelezo cha;

MAVAZI.
Mavazi ya wasichana yanasifa kuu mbili; kwanza ni mtindo (mshono) wa mavazi, pili ni usafi wa kawaida. Hivyo mtindo wa vazi na utunzaji wake hutazamwa sana na watu na hapo ndipo wataanza kukuweka katika makundi Fulani Fulani kulingana na muonekano wanje.

Je, haiwapasi watu wa mungu (wakristo) kuwa mfano wa kuigwa kwa muonekano wao wa nje na ndani? Ni vema kuwa kielelezo kwani katika mavazi kuna ujumbe unaowasilishwa kwa wengine”. Leo wamevumbua mishono mbalimbali yenye ujumbe yenye ujumbe kama vile sina adabu, simjali baba, sina kovu, wowowo na mishono mingi kama hiyo, ambayo shetani amekuwa akiitumia kudhalilisha uumbaji wa mungu na kuyapinga maandiko yanayosema, “uvae mavazi yanayositiri mwili” mitindo kama hii ni aibu kwa binti mkristo kuivaa, kwa mabinti wanaovaa mavazi kama haya, wanaonekana kuwa ni wahuni kwani inavaliwa na watu wenye sifa hiyo na hivyo hutashangaa kusikia mabinti hao wakipigiwa miluzi huko mtaani.

Mabinti wa kikristo wanashauriwa kuepuka mapambo mengi. Mavazi yachaguliwe kwa ajili ya uimara wake kuliko kwa kufanya maonesho. Mavazi yetu yaoneshe uzuri wa tabia ya mtu na yawe mavazi ya kawaida. “kufuatisha namna za walimwengu zisizo na kiasi katika mavazi ya wanaume na wanawake kunaonesha upungufu katika kuangalia mambo ya maana, kuna mavazi yasiyofaa na yanakiuka sheria za uadilifu, je wakristo waadventista wasabato wanayo kila sababu ya kujilinda na sheria ya uadilifu wasiwe wavunjaji wa maadili katika jamii.

Sababu kubwa ya kushamiri kwa ubakaji ni uvaaji mbovu wa mabinti ambao ni wabishi, wanaojitosa katika kuvaa mavazi hayo kama vipofu na wasiofikiri sawasawa madhara yake. Wengine huvaa mavazi ya sina adabu” au “simjali baba” mitindo ambayo huwafanya watembee mitaani wakionesha nguo zao za ndani jambo ambalo huamsha tamaa za wanaume na kuchochea ubakaji wa wanawake.
Mabinti wasio waungwana, huvaa mavazi yao na kuonesha nguo zao za ndani. Kwa binti je, anayosababu gani ya kuwafanya waoneshe nguo zao za ndani? kwani wao ni maduka?. Wengine wanavaa mitindo iitwayo “sina kovu” uvaaji huu ni wa kuhamasisha mazingira ya kupendwa ili waolewe. Badala yake wanaboresha mazingira ya zinaa na kubakwa. Ingekuwa kheri kwa wote wanaosikia ujumbe huu kubadili mitazamo yao mibaya ya kupenda mavazi hayo yasiyofaa wakristo tuwaachie watu wa ulimwengu wasio na nuru hii lakini sisi tuliopewa mwanga huu kwa neema ya yesu tubadilike tusaidie na wengine.

Miongoni mwa ujumbe tunaopata kutokana na mavazi ni kumtambua mtu kama kahaba” Mwanzo 38: 14-16 “huyo tamari akapewa habari, kusema mkweo anakwenda timna, akate manyoya ya kondoo wake. Basi akavua nguo za ujana wake, akajivika utaji, akajifunika uso, akakaa mlangoni pa Enaimu, karibu na njia ya kwenda timna, maana aliona kwamba shela amekuwa mtu mzima wala hakuozwa awe mkewe” “yuda alipomwona alimdhania kuwa ni kahaba, maana alikuwa amejifunika uso (nguo za kikahaba) Mithali 7: 10-11. Akamgeukia kando ya njia, akasema niruhusu niingie kwako. Maana hakujua ya kuwa ni mkwewe”. Hivyo tunaona mavazi ya kikahaba na mavazi ya kijana yalitambuliwa hata katika vizazi vilivyopita. Hivyo basi kuna mavazi ambayo binti akiyavaa yanaweza kumweka katika kundi la watu wa aina fulani na kufanya ajulikane kuwa ni mtu wa namna fulani. Pia yaweza kuongeza au kupunguza sifa ya binti.

Kwa ujumla tunaona kuwa makahaba walikuwa wakijulikana kwa mavazi yao. Mithali 7: 10-11. Je wewe mavazi yako yanayokufanya ujulikane kama nani ? Angalia sana mavazi yako yasije yakaharibu sifa yako njema. Mavazi yasiyofaa yanaharibu sifa njema ya mtu..

Naam japokuwa sisi siyo kile tunachovaa, kile tunachovaa kinaweza kueleza mengi kuhusu vile tulivyo; Kwa mantiki hiyo kama ilivyo kwa mifano yote, mavazi yanaweza kuwakilisha kitu kikubwa kuliko mavazi yenyewe, katika mavazi kama yalivyo mambo mengine tumejaliwa kumtukuza muumba wetu kwa usafi na yenye kukidhi afya yetu tena mazuri naya kufaa pia.

KANUNI YA MAVAZI:
Twafahamu tabia ya mtu kwa namna ya mavazi anayovaa.Mwanamke mwenye adabu, Mcha Mungu atavaa kwa adabu. Akili nzuri, moyo wa uadilifu, utadhihirishwa kwa kuchagua mavazi yanayofaa na yasiyo na mapambo mengi.Mtu asiye na kiburi katika mavazi yake na hali yake huonyesha kuwa mwanamke wa kweli huainishwa kwa uadilifu.

Nabii anasema; “Nawasihi watu wetu kuenenda kwa uangalifu na kwa tahadhari mbele za Mungu.Hebu dada zetu wavae pasipo urembo, kama wengi wafanyavyo, wakiwa na mavazi mazuri ya vitambaa vidumuvyo, ya kufaa siku hizi; Tena mavazi yasiwe jambo kubwa mawazoni. Yawapasa wajivike nguo za adabu, kusitiri aibu ya uchi na kuwa na kiasi. Wapeni walimwengu kielelezo cha nguvu cha kujipamba kwa neema ya Mungu. Wakristo wangemwiga kristo na kufanya uvaaji wao kupatana na neno la Mungu. Kwa unyenyekevu wangefuata unyofu, wasijali sifa, za kitambo na yafaa washikilie kutenda mema kwa sababu ya uzuri wa wema wao” Kutayarisha njia 1 (onyo juu ya mavazi UK.34.)

MAFUNDISHO YA BIBLIA. [ 1Timotheo 2;9,10, 1Petro 3;3-5 ]
v  Kristo aliona upendo wa mavazi, nae alionya, naam, akaamuru wafuasi wake wasiyafikiri sana hayo. “Na mavazi ya nini kuyasumbukia”usijisumbue kwa wakati wote kwa kujaribu kuiga namna  zote za mavazi zisizo na maana.vaa nguo safi na nzuri, lakini usijionyeshe ama kwa kuvaa maridadi, ama kwa kuvaa vibaya kwa uzembe. Tenda kana kwamba unajua kuwa jicho la mbingu linakutazama, na ya kuwa unaishi chini ya kibali cha Mungu ama kinyume na mapenzi yake.

Nabii anasema;nalielekezwa kwenye mafungu hayo juukiburi na upotevu wa mali katika mavazi ni dhambi ambayo mwanamke hupenda hasa. kiasi katika kuvaa ni wajibu wetu wa kikiristo, kuvaa bila kujipamba, kuepukana  na mavazi ya kubana, yasiyo na utukufu, yasiyo mafupi yanayodharirisha hekalu la Roho Mtakatifu kuwa kiwanda cha mvuto katika kutenda dhambi. Ni jambo linalopatana na IMANI YETU. Kutayarisha njia 1 (onyo juu ya mavazi)
        
KUCHUCHUMILIA VAZI LA KRISTO LILILO BORA ZAIDI.
v  Kiini safi cha upendo kitaipanua roho ya mtu ili kutoa nafasi kwa mambo bora zaidi kwa kutamani kuwa kama kristo na kutamani vazi la neema ya kristo yaani tabia yake na kuwa na mtindo wa maisha unaomtangaza kristo kama Bwana na Mwokozi wao kwa kupitia namna wanavyovaa.

Hatari kubwa ni kuwa wengi wanaojiita wakristo hawajui nguvu za roho ambazo wangeweza kupata kama wangetoa habari ya Ufalme wa Mungu kwa kupitia mavazi yao na kuonesha kielelezo cha kuwa Wana na Binti katika Ikulu ya Mfalme waliotayari kusimama katika Ikulu ya Mbinguni kwa namna wanavyovaa. Lakini jamii ya wakristo wengi wameridhika na hali ya kudumaa kiroho kwani wamejaribu Kutafuta kumtangaza shetani, dunia na mivuto na anasa zake kuwa bora zaidi kuliko Kristo, Mbingu na uzuri wake ambayo kristo ametuandalia na hili hudhihirishwa na maisha ya wakristo wengi.

v  Ndugu msidanganyike, mungu hadhihakiwi. Utakatifu tu, wala si kitu kingine, ndio utakaotufanya kuwa tayari kwenda mbinguni. Unyofu na Uchaji wa hakika katika mambo ya maisha ndio uwezo pekee wa kuwapa tabia safi, bora na kuwawezesha kuingia mbele za Mungu akaae penye nuru isiyoweza kukaribiwa.
Wanaume na wanawake walidhikao na tabia ya kudumaa na  kulemaa kiroho hawawezi kuingia mbinguni ikiwa hawezi kufanya Uamsho na Matengenezo haraka iwezekanavyo kwa kuacha mavazi yasiyomtangaza kristo. Tabia ya mbinguni lazima ipatikane hapa duniani ama sivyo haitapatikana kamwe na wengi tutapotea si kwa sababu hatupendi kwenda mbinguni bali tulipuuzia ujumbe wa wokovu na kuzidisha kiburi kwa mambo matakatifu.


MVUTO WA NAMNA YA MAVAZI.
v  Kupenda mavazi huhatarishatabia za uadilifu na kumfanya mwanamke kuwa kinyume cha mke mkristo mwenye adabu nay a kiasi. Mavazi ya kujionyesha, ya bei kubwa, mara nyingi huzidisha tamaa kwa mvaaji na kuamsha tama mbaya moyono mwa mtazamaji. Mungu anaona kuwa uharibifu wa tabia hutanguliwa na kuendekeza kiburi na umaridadi usio na maana.

v  Wengi wetu tumesahau kuwa Mungu ametuita kuwa mfano wa kurejesha  sura yake iliyopotea baada ya dhambi kuingia ni huzuni kubwa pale tunapovaa kama walimwengu wasioamini na kuongolewa na ulimwengu

v  Vijana wapendwa nia tuliyo nayo ya kuvaa kama mtindo wa siku hizi, watu wenye akili watahesabu jitihada zetu za mapambo ya nje kuwa ni Thibitisho la nia dhaifu tuliyo nayo na mioyo ya kiburi.

v  Kuna vazi ambalo kila mtoto na kijana anaweza kulitafuta na kulipata tu pasipokuwa na hatia. Hilo ni Haki ya Watakatifu, ikiwa tungekubali tu kufanya bidii kulipata vazi hilo kama tunavyojitahidi katika mitindo ya mavazi yetu kwa kuiga ulimwengu, Haingepita mda mrefu tungevikwa haki ya kristo na majina yetu hayangefutwa katika kitabu cha uzima.

v  Wakati mavazi ya dunia huchakaa mavazi bora ya Mungu huleta furaha, sifa na wokovu wa milele, hata hivyo lazima tuvae vazi la Mungu la wokovu ili tuweze kupata mibaraka anayoitoa.

v  Zekaria 3:4. Kuhani mkuu Yoshua anajikuta katiak mahakama ya hukumu akiwa na mavazi machafuakishitakiwa kwa dhambi zake zote. Hakimu wake, badala ya kumhukumu, anamvua mavazi achafu na kumvika mavazi safi na kumwita kuwa mtii.

v  Ikiwa kweli ujmbe wa Uamsho na Matengenezo umepokelewa na kristo kupokelewa katika mioyo ya watu kwa njia ya Roho Mtakatifu Uongofu wa kila kitu kisichopatana na Neno la Mungu kitaachwa. Lakini kama sivyo sauti hii itakuwa kama ukataji wa matawi {jambo ambalo si ufumbuzi wa kudumu kwani yatachipua tena} na kuzidi kutuvuta katika giza kuu.

v  Shetani nafurahia kuwavuta wengi kuwa tayari kwa pambano dhidi ya kristo kwa wengi kuwa tayari kupingana na mwonekano wa kristo katika dunia hii na hatari kuu inayoonekana kwa macho ya kiroho ni pambano hili kuwa sehemu ya kanisa leo ili Mlango wa Rehema ufungwe wakiwa na malumbano na kuacha kujiandaa kwa ujio wa kristo.

v  Mungu aliyewavika Adamu vazi la Utukufu alitegemea mwanadamu kuwa leo katika hali ya kuonyesha Utukufu wa Mungu hata kwa namna ya mavazi yake lakini kutokuwa na hofu ya Mungu Mwanadamu ametenda atakavyo kwa kufuata njia za ibilisi hivyo kuifanya Dhambi kuwa na Mvuto kuliko Utakaso.

v  Angalizo; wengi wamedanganywa na hali yao ya mioyo na kunukuu vifungu vya biblia kuwa kinga ya wao kutenda dhambi, hiyo ni dhambi kubwa sana kwani ni ya makusudi na inatumia vibaya maandiko Matakatifu. Ati Mungu haangalii nje( mavazi) isipokuwa mioyo kauli hii iko ndani ya biblia na shetani amewavuta wengi katika nyavu zake kwa nukuu hii na imekuwa tabia yake hata wakati wa yesu alisomewa kifungu cha biblia; Jibu ni kweli Mungu huangalia ndani ya moyo lakini Mungu akiwa ndani ya moyo Huwezi kuvaa mavazi yanayomtangaza vibaya Kristo.

SEHEMU YA PILI.
SOMO:   UTUNZAJI WA NYWELE.
Mungu alipomuumba mwanadamu alimaliza kila kitu na akaona ya kuwa ni chema sana, mungu alimwagiza mwanadamu kutunza kile alichopewa. Biblia inasema; lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake. Kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi  “(1kor. 11:15)”. Katika (1kor. 11:3), Biblia inasema, “lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanaume ni kristo na kichwa cha mwanamke ni mwanaume na kichwa cha kristo ni mungu” .
Unapomtazama mwanamume kichwani inatakiwa taswira ya kristo ndiyo ionekane, ukimtazama  mwanamke taswira ya mwanamume  ionekane kwake na utakapo mtazama kristo amuone mungu kichwani pake. (1 Kor.11:4), mwanamume hapaswi kufunika kichwa chake anaposali au kuhutubu maana anaaibisha kichwa chake “kila mwanamume asalipo au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaiibisha kichwa chake”. Anaaibisha kichwa kwasababu atakuwa amemfunika kristo ambaye anatakiwa kuonekana, ndiyo maana wanaume hawafuniki vichwa vyao hata kwa kuvaa kofia wanapokuwa kanisani au wasalipo maana kristo anapaswa kuonekana, utazamapo kichwa cha mwanaume.

Jambo hili ni tafauti kwa wanawake, (1 Kor.11:5) “bali kila mwanamke asalipo au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake kwa maana ni sawasawa na Yule aliyenyolewa”. Hapo maandiko yanaonesha kuwa, kwa mwanamke kufunika kichwa ni jambo sahihi na ndiyo maana hata leo katika makanisa yetu, tunashuhudia wakina mama wengi wao huingia kwenye ibada wakiwa wamefunika vichwa vyao kwa vitambaa lakini kwanini wamekuwepo ambao hawajafunika kwa vitambaa? Biblia inasema “…bila kufunika kichwa yuaaibisha kichwa chake, kwa maana ni sawasawa na Yule aliyenyolewa kumbe mwanamke akisali bila kufunika  kichwa ni sawa na Yule ambaye hajanyolewa ndipo anapaswa kufunika kichwa chake. Sasa tunatambua kwamba ambaye hajanyolewa ndipo anapaswa kufunika kichwa chake, sasa tunatambua kwamba ambaye hajanyolewa ni sawa kabisa na Yule ambaye amefunika kichwa, lakini asiyefunika kichwa ni sawa na aliyenyolewa. Kumbe nywele za mwanamke zinafunika kichwa chake sawa na yule aliyefunika kwa kitambaa. Hivyo tunaona si vyema kwa mwanamke kunyoa nywele zake maana zinahitajika ili zifunike kichwa chake ili mume wake aonekane, na kwa kuonekana kwa mwanamume kwenye kichwa cha mwanamke, kristo anaonekana, maana yeye hutawala  au kumiliki kichwa cha mwanamume, kupitia kwa kristo mungu huonekana.

Paulo aliwaambia wakorintho (1 kar 11:6), “maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe kauli ya Paulo ya kuwambia wakorintho “…mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele alisema hivyo huku akitambua kuwa kukatwa nywele katika jamii hiyo ni aibu hata wao wanafahamu, sasa ikiwa agizo la kufunika haliwezekani bora wakate jambo ambalo kwao haliwezekani kabisa, sasa kama kwao haliwezekani maana ni aibu ndipo Paulo anamalizia kwa kusema “….Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa na afunikwe  hii ilikuwa na namna ya kuendelea kusisitiza ufunikwaji wa nywele kwa wanawake maana hakuna njia nyingine.

Sababu zinazomfanya mwanamume asifunikwe kichwa na mwanamke kufunikwa kichwa zinaelewa wazi kuanzia (1 kor 11:7-10) mwanamume, haimpasi kufunikwa kichwa maana yeye ni mfano wa utukufu wa mungu, hivyo akifunikwa kichwa ni sawa na kuufunika utukufu wa mungu. Lakini mwanamke imempasa afunikwe kichwa ili utukufu wa mwanamume uonekana na huo ukionekana unamfunua kristo ambaye kupitia kwake utukufu wa mungu ndio unaoonekana (1 kor 11: 7-9).

Mwanamke anapofunikwa kichwa, anaonesha dalili ya kumilikiwa kichwani, si kwa ajili ya mwanaume tu bali kwa ajili ya malaika. Mtumishi wa mungu Paulo anauliza maswali ambayo majibu yake yanatupatia msimamo wa nini cha kufanya, Paulo anauliza, je! Inapendeza mwanamke amwombe Mungu asipofunikwa kichwa?, (1 kor 11:13). Jibu la swali hilo linapatikana katika (1 kor 11:5, 10). “Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa chake; kwa maana ni sawa sawa na yule aliyenyolewa kwa hiyo imempasa mwanamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani, kwa ajili ya Malaika.

Je! Mwanamuke naye anapaswa kuwa na nywele ndefu kama mwanaume? Mtumishi wa mungu Paulo anasema katika (1 kor 11:14), je! Hayo maumbile yenyewe hayawafundishi ya kwamba mwanake akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake?, Kwasababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi. Wanawake wanapaswa kuwa na nywele ndefu maana ni fahari kwao. Hapa Bibilia inaonesha kuwa haina ugomvi na mwanamke anayekuwa na nywele ndefu alizopewa na Mungu ili ziwe badala ya mavazi yaani mavazi ya kufunika kichwani. Hivyo mwenye nywele ndefu ni sawa tu na yule aliye na mavazi ya kufunikia kichwani. Mungu amewapatia wanawake nywele ndefu ili ziwaongezee fahari, sasa kama nywele hizo umepewa na Mungu, unapaswa kuzitunza. Hapa Bibilia inazungumzia nywele ambazo mwanamke amepewa na Mungu, wala Bibilia haijataja wala hajamaanisha nywele za bandia. Fungu linasema lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni fahari kwake, kwa sababu amepewa zile nywele ndefu ili ziwe badala ya mavazi (1 kor 11:15)”. Jiulize swali hili, je, nywele ulizo nazo umepewa na Mungu au umepewa na wachina (wazungu).

MWENDELEZO WA SEHEMU YA TATU 
.
SOMO: NI KUPAMBA? AU NI KUTUNZA NYWELE.
Wanawake wanashindwa kutofautisha kati ya “kutunza nywele” na “kupamba nywele “lazima utofautishe kati ya kutunza na kupamba.
Kamusi ya Kiswahili sanifu inatoa maana ya maneno haya:
Kutunza” maana yake ni kukiweka kitu katika hali nzuri ili kisiharibike.
Kupamba” maana yake ni kuweka urembo au nakshi zaidi ya kawaida yake.
Wasichana wengi na wanawake kwa ujumla katika ulimwengu huu wa leo wameamua kupamba nywele zao badala ya kuzitunza. Kupamba nywele  kunaweza kuwa na hasara kadha wa kadha ambazo huambatana na matumizi ya vitu vitumikavyo kupambia nywele hizo. Hasara hizo ni za kiuchumi na kiafya lakini hasara nyingine kubwa ni hasara ya kiroho.

(a)  Madhara ya Kiuchumi.

i.             Gharama kubwa katika kupamba nywele. Wanawake wengi wanatumia pesa nyingi kununua mapambo ya nywele, kwenda saluni, na kuwalipa mafundi wa kuzilemba na kuzipamba. Wanadhani kwa kufanya hivyo watapendeza na kuongeza kukubalika kwao, kumbe wanajiweka katika sehemu mbaya mno. Wavulana wazuri japo hawawaambii waziwazi, wanawaogopa wasichana hao kwa sababu wamejiweka katika daraja la watu wa gharama kubwa. Vijana hao wa kiume huwa wanawakwepa kwa kuhofia gharama za kupamba nywele za mwanamke huyo.

ii.           Kupamba nywele kunahitaji muda wa kutosha ili kuzishughulikia. Muda mwingi ambao ungeweza kutumika kwa shughuli nyingine za kimaendeleo, unapotezwa kenye upambaji wa nywele. Kama muda huo ungelitumika kuzalisha au kufanya kazi fuluni ya kiuchumi basi wanawake hao wangepunguza gharama kubwa za maisha na kuongeza uzalishaji kwa matumizi mazuri ya muda.

(b)  Madhara ya kiafya: 

MADHARA YA KIAFYA YANAYOTOKANA NA MATUMIZI YA VIPODOZI.
Mamlaka ya madawa na chakula (marekani) imetafsiri vipodozi kama kemikali ambazo hutumika mwilini kwa lengo la kuosha, kuongeza uzuri na mvuto bila kuharibu kiungo cha mwili na kazi yake. Kwa lugha rahisi vipodozi hubadilisha muonekano wa mtumiaji. Vipodozi huhusisha; kemikali za ngozi, “lotion”, poda, marashi (perfumes), mafuta ya mdomo (lip sticks and lip shine), rangi za kucha, kemikali za uso na macho (eye and facial make up), rangi za nywele (hair colours), marashi ya nywele (hair spray and gels), mafuta ya kuogea na michoro ya mwili (tattoos).

Baadhi ya kemikali (ingredients) za vipodozi zenye madhara mwilini ni;
(i)           Rangi za kucha zina kemikali iitwayo “sodium lauryl sulfate” ambayo husababisha ugonjwa wa ngozi (dermatitis).
(ii)           Kutumia “make up” kwa muda mrefu husababisha ugonjwa wa nywele za kope (eyelashes), ambao humfanya mtumiaji awe na hatari ya kupata ugonjwa wa macho (keratitis).
(iii)        Kemikali zinazotumika kutunza vipodozi (preservatives) kama “ureas” zinasababisha ugonjwa wa ngozi (dermatitis). Aidha kemikali zingine kama methyl, propyl na butyl zinaweza kusababisha saratani ya matiti (breast cancer).
(iv)         Vipodozi vinavyotokana na “petrol” au “paraffin” vinaziba vitundu
vidogo vidogo vya ngozi na kufanya ngozi isitoe uchafu vizuri na hivyo kusababisha chunusi.
(v)          Kemikali kama “oxybenzone” na “octylmethoxycinnamate” inaharibu mfumo wa hormone, hivyo kuathiri shughuli za kikemikali za mwili.
(vi)         “propylene glycol” inasababisha matatizo ya macho, saratani, inaathiri uzazi (wajawazito) na pia ni sumu endapo mtu atakunywa kwa bahati mbaya.
(vii)       “sodium lauryl sulphate” inayowekwa kwenye cream nyingi na shampoo inasababisha ngozi kuwasha, huingia mwilini kwa urahisi na hukusanyika kwenye jicho, ubongo, moyo na ini kwa muda mrefu, hivyo kuathiri utendaji wa viungo hivyo.
(viii)     Rangi za vipodozi zinasababisha saratani.
(ix)        Marashi (perfumes). Perfume (1) inaweza kutengenezwa na kemikali  hadi 200. Baadhi ya kemikali hizo husababisha maumivu ya kichwa, kizunguzungu, chunusi, kukohoa, ngozi kuwasha, aleji na kutapika.
(x)          Kemikali nyingi huharibu na kuondoa seli (cells) za ngozi zilizokomaa (melanin) na kuacha seli zilizo changa; hivyo kuathiri ulinzi ambao  ngozi huutoa dhidi ya vimelea vya magonjwa na mionzi ya jua. Kwa hali hii mwili upo hatarini kushambuliwa na vimelea vya magonjwa, saratani ya ngozi na kuumia kwa urahisi.
Kwa ufupi; kemikali (ingredients) zifuatazo ni htari kwa afya yako; methyl, propyl, butyl, ethyl diethanolamine (DEA) or Triethanolamine (TEA), Diazolidinyl urea, sodium lauryl, petrolatum, synthetic colours e.t.c
Lakini pia kemikali ya Methylmercury inoyotumika kwenye vipodozi na kemikali za kukuzia nywele ina madhara yafuatayo;
(a)  Kwa vitoto ambavyo bado viko tumboni (fetus), watoto wachanga waliozaliwa (infants) na watoto wakubwa kidogo (children), hupata madhara ya vipodozi hivyo kupitia mama zao wakiwa tumboni. Madhara hayo ni pamoja na kuadhiri ukuaji wa ubongo wa mtoto na mifumo ya mwili (effects on baby’s growing brain and nevous system).
(b)   It also affects peripheral vision and disturbances in the body, especially sensations (hisia katika) in the hands (mikono), feet (miguu) and around the mouth (maeneo ya midomo).
(c)  Lack of coordination movement (kuharibu mwondoko wa mwili); impairment (madhara katika) of speech (kuogea), hearing (kusikia), walking (kutembea) and muscle weakness (uthaifu wa misuli).
(d)  Husababisha ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi, saratani ya ngozi, saratani ya mifupa, saratani ya damu. Ingawa ugonjwa huchukuwa muda mrefu kudhihirika.
(e)  Disturbances in sensation, (kuharibu mifumo ya hisia ya ngozi).
(f)   Changes in never responses,(mabadiliko katika mwitikio wa neva).
(g)  Performance deficits on tests of cognitive function,(kuharibu uwezo wa kuelewa).
(h) Kidney effects, (madhara ya figo)
(i)   Respiratory failure,(kuathiri mifumo ya upumuaji).
(j)   Death,(hupelekea kifo).
(k)  Skin rashes and dermatitis, (michubuko ya ngozi na muwasho).
(l)   Mood swings, (kubadilika kwa hali ya mtu ovyo bila sababu)
(m)               Memory loss, (kupoteza uwezo wa kumbukumbu).
(n)  Mental disturbances, (kuvurugika akili).
(o)  Muscle weakness.
Walioadhirika na matatizo hayo waonane na wataalam wa Afya kwa msaada zaidi. Makampuni mengi hayaorodheshi kemikali zote zilizotumika kutengeneza vipodozi hususani  zenye madhara makubwa. Bidhaa nyingi zinapambwa kwa majina mazuri kama “natural” ama “organic” wakati zinamadhara makubwa kiafya.

TAARIFA YA WIZARA YA AFYA (2004) KATIKA HOSPITALI ZIFUATAZO:
Hospitali ya Mirembe na Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI).
Hospitali ya Mirembe inahudumia wagonjwa wenye matatizo ya akili, wakati hospitali ya oceanroad inhudumia wagonjwa walioathirika na magonjwa ya saratani. Kumbuka mpendwa hayo ni magonjwa yanayosababishwa kwa kiasi kikubwa na utumiaji wa kemikali katika vipodozi, ambapo athari zake huanza kuathiri mtoto akiwa bado yuko tumboni.

Hospitali ya Mirembe hutoa huduma za rufaa kwa wagonjwa wa magonjwa ya Akili. Katika mwaka 2004 iliweza kutoa huduma ya wagonjwa wa nje 33,067 na waliolazwa 3,010. Idadi ya vifo vilivyotokea katika mwaka 2004 kwa wagonjwa wa magonjwa ya akili ilikuwa asilima 4.4 ya idadi ya wagonjwa waliolazwa.
Magonjwa ya Akili kumi yaliyoongoza kwa wagonjwa waliolazwa mwaka wa 2004 ni Schizophrenia 61%, Epilepsy 229 (8.4)%, Organic brain syndrome 134 (6%), Acute psychosis, Psychoactive substance use disorders 14% Depression, Alcoholic psychosis 2% Manic-depressive psychosis, Mania 0.7%, Senile dementia 1.4%, Acute Psychosis 0.9%, Mental deficiency 0.5% na Anxiety neurosis 0.4%

Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI)
Taasisi ya saratani ocean road ni taasisi maalum ya kutibu magonjwa ya Saratani, kwa mwaka 2004 ilihudumia wagonjwa wa nje (OPD) 6,962 ambapo wagonjwa 2,947 walikuwa wa Saratani ya shingo ya uzazi na kati ya hao wagonjwa wapya walikuwa 992 na waliokuwa wakifuatiliwa ni 1,955. Wagonjwa 4,015 walikuwa na Saratani za aina nyingine ambapo 1,874 kati yao ni wapya na 2,141 walikuwa wakifuatiliwa.

Kuhusu wagonjwa, wagonjwa 2,312 walilazwa mwaka 2004. Jumla ya vifo 187 vilitokea kutokana na magonjwa ya Saratani. Saratani ya shingo ya uzazi iliongoza kwa 34.6% ikifuatiwa na Kaposis Sarcoma 14%, Oesophagial carcinoma 8.1 %, Saratani ya matiti 8.0 % pamoja na Saratani za Head and Neck 7.8% kati ya magonjwa kumi yaliyooongoza kwa magonjwa ya nje (OPD). Tiba ya mionzi ilitolewa kwa wagonjwa 30,045 ambapo Shingo ya uzazi ilioongoza katika viungo vilivyotibiwa kwa 65%, ikifutiwa na Head and Neck 10.5% pamoja na Oesophagus 6.3%. Zingatia idadi ya wagonjwa waliohudumiwa, waliokufa, jumla yao walioadhirika. Tazama pia magonjwa yaliyowafanya wengi kulazwa katika taasisi hizo za Afya. Utagundua kuwa vyanzo vya magonjwa hayo vinapatikana ndani ya vipodozi vinavyoonekana kupendwa na kutumiwa na wanawake wengi. Je, watumiaji watapona kwa hali hii, mabadiliko yasipofanyika?

Wapenzi watu wa Mungu, hata katika nchi ya Tanzania, Mamlaka ya chakula na Dawa (TFDA), imepiga marufuku baadhi ya vipodozi ambavyo vimeonekana kuwa na madhara makubwa kwa binadamu. Ikiwa taasisi hii yaweza kuwa na kitu chema cha kuionya jamii inayotumia vipodozi kumkosoa Mungu katika uumbaji wake, habari gani kwa sisi watu wenye nuru ya Mungu?. Kwanini tusiridhike na jinsi Mungu alivyotuumba? Huko ni kuwaka tamaa na kukosa kuwa na kiasi, ndipo tunafikiria kumkosoa Mungu katika uumbaji wake. Wanawake wanajiwekea makalio yasiyo yao, kupunguza matiti au kuyapandisha, kupaka rangi za kucha, mdomo na sehemu nyingine, kutumia dawa za kuongeza hips, kutumia dawa za kukuza nywele, kuweka nywele za bandia na kukoboa ngozi. Tusipo isikia sauti ya Mungu inayotuita leo kutoka Babeli, tutaangamia kwa magonjwa yaliyotajwa hapo juu, ambayo chanzo chake kikubwa ni matumizi ya hivyo vipodozi.

Soma taarifa ya gazeti hili la Mwananchi hapo chini, iliyoripotiwa 24 May 2012 20:48
MWANANCHI:

Thursday, 24 May 2012 20:48
Daniel Mjema, Moshi
WAKATI Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), ikipiga marufuku matumizi ya vipodozi hatari kwa afya za binadamu, vipodozi hivyo sasa vimetapakaa katika maduka mbalimbali ya vipodozi mkoani Kilimanjaro.
Hali ni mbaya zaidi katika mji wa Moshi na vitongoji vyake ambapo baadhi ya Maofisa wa Afya wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, wamegeuza biashara hiyo kuwa mradi ambapo ‘humalizana’ kiaina na wamiliki wa maduka hayo.
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini baadhi ya maduka hayo kuuza  vipodozi hivyo kwa usiri mkubwa kwa kutazama sura ya mteja ambapo sehemu kubwa ya wale wanaouziwa ni wanawake  huku wanaume wakitiliwa mashaka.

Vipodozi vilivyozagaa kwa wingi ni Carolight, Mekako, Maxi Light, Bio Carote, Carottene na G&G cream, Rico Cream, Princes Cream na Clare Cream ambavyo TFDA ilitangaza vipodozi hivyo kuwa na madhara makubwa kwa binadamu.

Maduka yaliyosheheni vipodozi hivyo yapo katika stendi kuu ya mabasi Moshi Mjini, stendi ya Soweto, Barabara ya Nyerere maarufu kama Double Road, maeneo ya KCMC na baadhi ya maduka ya bidhaa za rejareja yaliyopo kwenye makazi ya watu.

Katika kuthibitisha kuzagaa kwa vipodozi hivyo, mwandishi wa habari hizi aliamua kumkodi  mwanamke mmoja na kuzunguka naye katika maduka sita kununua vipodozi hivyo na akauziwa japo vilikuwa vikichukuliwa nje ya makabati ya bidhaa.

Habari zaidi zilidai kuwa Afisa mmoja wa Afya katika Manispaa ya Moshi(jina tunalo) amekuwa akipita katika maduka hayo mara moja au mbili kwa mwezi na kuchukua hongo ya kati ya sh100,000 na sh200,000 kwa kila duka.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi, Dk. Christopher Mtamakaya alipoulizwa jana alisema hana taarifa juu ya kuzagaa kwa vipodozi hivyo na kuahidi kufanya operesheni ya kukagua maduka yote ya vipodozi.

Tayari TFDA ilishatoa taarifa kwa umma juu ya kuwepo kwa vipodozi karibu 200 ambavyo vimetengenezwa kwa madini hatari ya Hydroquinine, Steroids, Bithionol na Zebaki ambayo yana madhara makubwa kwa binadamu.
Taarifa hiyo ya TFDA inasema vipodozi hivyo hatari huweza kusababisha kansa ya ngozi kwa mtumiaji, akina mama kuzaa watoto wenye mtindio wa ubongo na uharibifu wa ini na figo na athari huchukua muda mrefu kutambuliwa.

Historia ya upambaji wa nywele katika Biblia.
Katika bibilia upambaji wa nywele uliambatana na wanawake waovu, wauaji, Malaya na wenye mashetani au waabudu mashetani. Kisa cha Yezebeli katika (2 Falme 9:30), kina onesha kuwa Yezebeli alizaliwa katika Ikulu ya sidoni katika nyumba ya waabudu mashetani au miungu. Miungu yao ilikuwa “ Baali au Bel” mungu mkuu wa kiume aliyeabudiwa kwa kutoa kafara za wanadamu. Bibilia inashuhudia ibada ya namna hiyo. Nao wamemjengea Baali mahali pake palipo juu ili kuwachoma moto wana wao wawe sadaka za kuteketezwa kwa Baali (yer 19:5) kando ya ibada hiyo ya kuchoma watoto, ilijumuisha uasharati.

Yezebeli akaolewa na Ahabu mfalme wa Israel. Binti huyu hakuacha ibada ya Baali katika taifa la Israel (1falme 18:4). Hivyo wale wanaooa mabinti wanao jipamba wakidhani watawabadilisha wanajidanganya huko ni kuleta moto wa kigeni katika familia yako na ndipo mtaungana kuabudu miungu mingine.

Lakini Yezebeli alikuwa mwongo na muuaji pia, (1 falme 21:1-16), ndipo baada ya miaka kadhaa, Yehu akaenda kulipiza kisasi, akamkuta huyu mwanamke na tabia yake ya kupamba nywele, Bibilia inasema Yezebeli akapata habari akatia wanja akapamba kichwa chake ………(2 falme 9: 30), lengo lake la kufanya hivi kwanza aliamini miungu yake itamsaidia lakini pia alitaka Yehu amtamani ili asimuue. Lakini Yehu alipomwona hakumhurumia alimuua (2 Falme 9:33).

Kwahiyo tunaona kuwa upambaji wa nywele si wa wanawake wa kristo. Bali kiasilia ni wa waabudu mashetani ambao huenda sambamba na uovu, uuaji na uasherati. Kuweka nywele za badia zilizo na rasta, kuweka rangi (nyekundu, nyeupe au kahawia na kadhalika) na kuweka wanja, hayo yana kutia hasara kiuchumi, lakini pia yanaharibu sifa yako njema ya kiroho.

Ndugu wapenzi katika kristo nawasihi kwa neema ya Yesu epukeni kupamba nywele maana hayo ni kwa waabudu mashetani. Mungu anachotuagiza kufanya ni kutunza na wala sio kupamba nywele. “kujipamba kwenu kusiwe kujipamba kwa nje, yaani kusuka nywele na kujitia dhahabu na kuvalia mavazi(1peter.3:3).” kumbuka hapa maandiko yanazungumzia kupamba si kutunza. Mapambo yanayo kubaliwa hapa na ndiyo yanayo zungumzwa ni mapambo yasiyo haribika, yaani roho ya utulivu maana ndivyo walivyo jipamba wanawake watakatifu wa zamani (1 pet.3:4).

Katika ufunuo 2:20 anatajwa mwanamke kwa kuhusika na uovu kama uzinzi , lakini nina neno juu yako  ya kwamba wamridhia Yule mwanamke Yezebeli yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watu wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu”. pia mwanamke wa ufunuo 17 naye pia ameonekana amepambwa lakini anatajwa kuwa mzinzi huwakilisha kanisa lililo asi.

Kwa hiyo ili nywele zako zikupatie heshima na kuvutia kukubalika kwako zitunze katika hali ya usafi usiziache zikakuletea usumbufu kichwani kama vile kuwasha na kuwa makao ya chawa na uchafu. Kwa kuziweka nywele katika hali nzuri inakulazimu kuziosha vizuri mara kwa mara kwa sabuni. Baada ya kuziosha zipake mafuta maalum ya nywele, sio madawa. Usiache nywele zako zinasokotana na kufanya zisipendeze, na unapojaribu kuzichana zinauma. Osha, paka mafuta na zichane. Biblia inasema wala kichwa chako kisikose marhamu (Muhubiri 9:8).” Kwa nini wewe unaacha nywele zako kuwa chafu? Jaribu kutumia nywele zako kujipatia sifa njema, kanisani, nyumbani, shuleni, chuoni, au katika jamii inayokuzunguka. Jiepushe na mitindo isiyompa Mungu utukufu.

HITIMISHO:
MSIMAMO WA KANISA, THISDASO T.U, THISDASO DODOMA ZONE.
1kor.4:1 – Mtu na atuhesabu hivi; kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu. Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.

Kwakweli kama wakristo, tunayo kila sababu ya kuwa kielelezo katika maeneo tunayoishi ili kuwa nuru kwa watu wengine wanaoteseka na mambo ya Dunia hii yasiyo na faida. “Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na Neno hili, bilishaka kwa hao hakuna asubuhi” (Isaya 8:20). Kama wakristo ikiwa hatuendi sawasawa na Neno sisi kwetu hakuna asubuhi, maana hatutakuwa nuru kwa wtu.

Watu wa Mungu huongozwa na Neno la Mungu, ili liwakinge katika kushindana na mivuto ya walimu wadanganyifu na nguvu za uongo wa pepo za giza. Shetani anatumia kila hila awezayo kuwazuia ili awazuie watu kufahamu maarifa ya Biblia. Katika kila uamsho wa kazi ya Mungu, mkuu wa uovu huamka kufanya bidii zaidi; anajitahidi kupita kiasi kushindana na kristo na wafuasi wake. Angalia sana pepo hili baya la ibilisi la kutaka kukwamisha kazi ya Mungu lisikutumie kwa kazi zake, tumwombe Mungu atupatie uwezo wa kuzipinga hila za shetani, Tule kwa kiasi, Tunywe kwa kiasi, Tuhusiane kwa kiasi, Tuvae kwa kiasi, Tuongee kwa kiasi huku tukijua kuwa sisi ni chumvi ya Dunia. 

Hii ni saa ya hatari kubwa.
Kitakacho vumilia mapigo saba ya mwisho ni tabia iliyo takatifu. Hitaji muhimu……Hitaji kubwa la kanisa la masalio si ongezeko la washiriki, wahubiri zaidi, au vifaa zaidi. Zaidi sasa hitaji kubwa leo ni watu waume na wake waliojazwa na Roho Mtakatifu. Kumaliza kazi ya Mungu, yatupasa tupokee kwa upya kila siku ubatizo wa Roho Mtakatifu.

“Hakuna hata mmoja anayedai utakatifu ambaye ni mtakatifu wa kweli. Wale ambao wameandikwa kuwa ni watakatifu katika vitabu vya Mbinguni hawajifahamu, nao huwa ni wa mwisho kujivunia wema wao wenyewe”.

“Wale ambao kwa kweli wanatafuta kukamilisha tabia zao za Kikristo hawatakubali kuwalazimu kuwa hawana dhambi. Maisha yao yanaweza kuwa hayana hatia, wanaweza kuishi maisha yanayowakilisha kweli walioipokea, kwa kadri wanavyoweka mawazo yao kudumu kwenye tabia ya kristo, kwa kadri wanavyokaribia sura yake ya kimungu….”watakamilishwa nao watayachukia mambo ya dunia hii yanayoonekana kuwavutia walio wengi.

Wale wanaojaribiwa kumsaidia Shetani kulaumu viongozi na washiriki katika kanisa la masalio, watafanya vyema kutafakari maonyo ya ujumbe wa Mungu katika mafungu yafuatayo; 6 T 42 – “Hhakuna chochote katika ulimwengu huu kinachopendwa kama Kanisa la Mungu. Mungu ana kanisa ulimwenguni, ambao ni watu wake waliochaguliwa wanaozishika amri zake. Anaongoza, si machipukizi yanayofarakana, si mmoja hapa na pale, lakini watu waliopamoja”. (kutayarisha njia sehemu ya pili, u.k 48).

“Hakuna kinacho mkosea Mungu kama tendo la kudharau mvuto wa wale wanaoifanya kazi yake. Atawahesabia kosa wale wote wanaomsaidia Shetani katika kazi yake ya kulaumu na kukatisha tama” (kutayarisha njia sehemu ya pili, u.k 48). “Yatupasa tuwe na bidii kubwa. Hatuna muda wa kutumia kwa kulaumu na kutoa mashitaka. (kutayarisha njia sehemu ya pili, u.k 48). “Lolote lililo baya, la chuki, kulaumu, kudhulumu, hayo si ya kristo, bali hutoka kwa Shetani” (kutayarisha njia sehemu ya pili uk 48)

“Kuvutwa kuingia katika kulaumu wengine, kungekuwa ni ishara ya hatari kwetu, kwani roho mtakatifu anapotutakasa na kutubadilisha, mioyo yetu itajazwa na upendo kwa ndugu zetu….” “Ijapokuwa ni kweli kwamba wengi wetu katika kanisa la Masalio wako katika hali ya Laodikia, ambao wengi watatikiswa na kutolewa, hata hivyo kanisa wako walio waaminifu ambao watasikia mashauri ya Kristo aliye Shahidi wa kweli…watatayarishwa kwa mvua ya masika, wakishiriki katika kutoa ujumbe pamoja na Kilio Kikuu na kuwa tayari kubadilishwa.

“Hili ni kanisa la Masalio. Mungu hataongoza kanisa lingine. Sasa ni wakati wa kujitayarisha kwa mvua ya masika. Na tungekumbuka kila siku kuwa kazi hii ya kujitayarisha yapasa ianze wakati wa mvua ya vuli” (kutayarisha njia sehemu ya pili uk 48)
Furaha yetu ya baadaye inategemea kuwa ubinadamu wetu, na uwezo wake wote, view katika kumtii Mungu na kuweka chini ya utawala wa Kimungu…” “Kristo anatamani kuwa kila mmoja wetu akate shauri mapema” “Bidii isiyo na kikomo ingekuwa yetu sasa”
Mwisho.
“Ombeni kuwa nguvu ya Roho Mtakatifu, ikiwa na uwezo wake mwenyezi, unaohuisha na kugeuza, uijie roho iliyolemaa kama nguvu ya umeme ikiufanya kila mshipa kuamka kwa uzima mpya, kumhuisha mwanadamu kutoka kwa ufu wake wa kidunia na hali ya kimwili”.
Mungu awabariki mnapojiandaa kila mmoja wetu kufanya mabadiliko kwa yale ambayo Roho amekushuhudia kupitia somo hili ya kwamba ufanye matengenezo.


BWANA AWABARIKI.
Somo hili imeandaliwa na mainjiristi wafuatao;
-CHERLES ANTHONY. (MSAIDIZI M/KIROHO THISDASO DODOMA ZONE).
-MOGENGE EMMANUE S. (MKUU M/KIROHO - THISDASO DODOMA ZONE).
-GIDION HABILI. (M/KITI – THISDASO DODOMA ZONE).
- KESHI MARTIN MALEHIWA. (M/KITI - THISDASO TANZANIA UNION).

VIELELEZO VYA NUKUU
CD    - Counsels or Diet and Foods.
Te      - Temperance.
T       - Testimonies for the church Volume I
MH    - The Ministry of Healing
PP     - Patriarchs and Prophets
CS     - Counsels on Stewardship
Ed     - Education.
         -Nusuru Ndoa yako. By Pr.Makoye
         -Kuchagua Mchumba. By E.G White
         -kutayarisha njia sehemu ya pili.
Limeandaliwa na Emmanuel Mogenge THISDASO DODOMA ZONE.


No comments:

Post a Comment